< 1 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
Paul, Silvanus et Timothée à l'église des Thessaloniciens en Dieu le Père et en Jésus-Christ le Seigneur. Grâce et paix vous soient accordées.
2 Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
Nous rendons constamment grâces à Dieu pour vous tous; nous vous nommons dans nos prières;
3 Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
et nous rappelons sans cesse, en présence de Dieu notre Père, les oeuvres de votre foi, les travaux de votre charité et la persévérance de votre espoir en notre Seigneur Jésus-Christ.
4 Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
Nous savons, frères bien-aimés de Dieu, que vous avez été élus;
5 maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
car nous ne vous avons pas évangélisés seulement avec des paroles, mais avec une vraie puissance, avec l'Esprit saint, avec une forte conviction. Vous savez bien ce que nous avons été au milieu de vous et pour votre bien,
6 Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
et vous êtes devenus nos imitateurs et ceux du Seigneur, en accueillant sa parole dans un moment de grande affliction avec la joie que donne l'Esprit saint.
7 Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
Aussi êtes-vous devenus un modèle pour tous les croyants de la Macédoine et de l'Achaïe.
8 Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
Car c'est de chez vous que la parole du Seigneur s'est fait entendre; et ce n'est pas seulement en Macédoine et en Achaïe, c'est partout que votre foi en Dieu a été connue; aussi n'avons-nous pas besoin d'en parler.
9 Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
Chacun raconte en parlant de nous comment vous nous avez reçus à notre arrivée, comment vous vous êtes convertis à Dieu, abandonnant les idoles pour le servir, lui, le Dieu vivant et vrai,
10 na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.
et pour attendre du haut des cieux son Fils qu'il a ressuscité des morts, Jésus, celui qui nous délivre de la colère à venir.

< 1 Wathesalonike 1 >