< 2 Wakorintho 12 >

1 Nitajivuna basi, ingawa haifai! Lakini sasa nitasema juu ya maono na ufunuo alivyonijalia Bwana.
ninoghiile kukughinia nambe nakuvumbulila kimonga. looli nitapikughinia vwimila inyivonelo ni mhola isingi sino ambonisie uMutwa.
2 Namjua mtu mmoja Mkristo, ambaye miaka kumi na minne iliyopita alinyakuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
nimmanyile umuunhu jumo mwa Kilisite, juno amaka kijigho na ghane gha kilile, alyatolilue kuhanga kufika ku vulanga uvwa kukyanya fiijo. — apuo nanikagwile pamo alyale mu m'bili ughu, pamo naalyale mu m'bili ughu, looli uNguluve ghwemwene akagwile.
3 Narudia: najua kwamba mtu huyo alinyakuliwa mpaka peponi. (Lakini sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
kange nikagwile kuuti umuunhu uju - pamo alyale mu m'bili ughu, pamo naalyale mu m'bili ughu, une nanikagwile, looli uNguluve ghwe mwene akagwile.
4 Huko akasikia mambo ya siri ambayo binadamu hastahili kuyatamka.
alyatolilue kuhanga kufika ku paladiso ukuo akapulika amasio amimike kyongo ghano umuunhu naangajove kange naanoghile kujova.
5 Basi, nitajivunia juu ya mtu wa namna hiyo, na si juu yangu mimi binafsi, isipokuwa tu juu ya udhaifu wangu.
lino nikughinia vwimila umuunhu ujuo. une nanikughinia vule nilivuo, ulwene nikughinia vwimila uvuvotevote vwango.
6 Kama ningetaka kujivuna singekuwa mpumbavu hata kidogo, maana ningekuwa nasema ukweli mtupu. Lakini sitajivuna; sipendi mtu anifikirie zaidi ya vile anavyoona na kusikia kutoka kwangu.
nambe naale nilondaghe kukughinia, naale niiva n'jaasu, ulwakuva naale niiva nijova isa kyang'haani. lino nikusigha kukughinia, kuuti umuunhu ghweni alekaghe kukumbona une kuuti ninoghiile kyongo kukila sino vikusivona na kukusipulika kuhuma kulyune.
7 Lakini, kusudi mambo haya makuu niliyofunuliwa yasinifanye nilewe majivuno, nilipewa maumivu mwilini kama mwiba, mjumbe wa Shetani mwenye kunipiga nisijivune kupita kiasi.
neke kuuti nileke kukughinia kyongo vwimila inyinga isa kudegha sino uMutwa uYeesu ambonisie, nikapelua ulupumuko mum'bili ghwango luno luli ghwene mafua. ulupumuko uluo nsung'hua ghwa Setano, asung”hilue kuuti amhumhusie, neke nileke kukughinia.
8 Nilimsihi Bwana mara tatu kuhusu jambo hili ili linitoke.
nikansuuma uMutwa katatu kuuti amhoke mulupumuko uluo.
9 Lakini akaniambia: “Neema yangu inatosha kwa ajili yako; maana uwezo wangu hukamilishwa zaidi katika udhaifu.” Basi, ni radhi kabisa kujivunia udhaifu wangu ili uwezo wake Kristo ukae juu yangu.
neke umwenen akam'buula akati, ulusungu lwango lukukukwila, ulwakuva muvuvotevote mwe muno ingufu sango sivoneka. mu uluo nikughiniagha nu lukeelo ulukome vimila uvuvotevote vwango, kuuti ingufu sa Kilisite sivisaghe numue.
10 Kwa hiyo nakubali kwa radhi udhaifu, madharau, taabu, udhalimu na mateso, kwa ajili ya Kristo; maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.
lino nili nulukeelo vwimila uvuvotevote, kulighua, kuuva mu nhalamu, kuuva mulupumuko na kuhangajisivua vwimila uKilisite, ulwakuva pano niiva m'botevote, pe pano niiva ni ngufu.
11 Nimekuwa kama mpumbavu, lakini, ninyi mmenilazimisha kuwa hivyo. Ninyi ndio mngalipaswa kunisifu. Maana, ingawa mimi si kitu, kwa vyovyote, mimi si mdogo zaidi kuliko hao “mitume wakuu.”
lino une nili n'jaasu umue mwemue mumheliile ku ulu. umue muveela munoghile kukunginia, ulwakuva nambe nivoneka kuuti naninoghiile, une nanili nsunghua n'debe kukila avuo vano vitambulua vasung'hua vavaha.
12 Miujiza na maajabu yaonyeshayo wazi kwamba mimi ni mtume yalifanyika miongoni mwenu kwa uvumilivu wote.
ye nili ku lyumue nikaale nu lugudo na kuvomba ifidegho ni fi valilo fino fyahufyagha kuuti une nili nsung'hua.
13 Je, mlipungukiwa nini zaidi kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi kwa upande wangu sikuwasumbueni kupata msaada wenu? Samahani kwa kuwakoseeni haki hiyo!
nakwekili kimonga kino nivombile kufipugha ifingi ifya vitiki. neke nanivombile kulyumue. ulwene kuuti pano nanikaale n'sigho kulyumue? neke uvuo vwe vwitiki vwango, mun'saghilaghe.
14 Sasa niko tayari kabisa kuja kwenu mara ya tatu, na sitawasumbua. Maana ninachotafuta si mali zenu, bali ni ninyi wenyewe. Ni kawaida ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba, na si watoto kuwawekea wazazi wao.
lolagha! une nikulinga'hania kukwisa kulyumue ulwa vutatu. neke naningave n'sigho kulyumue ulwakuva nanilonda ifiinu fiinu, nikuvalonda umue. ulwakuva avaanha navanoghiile kuvuta ifiinu kuuti five fya vapafi, looli avapafi vanoghiile kuvuta ifiinu kuuti five fya vaanha.
15 Mimi ni radhi kabisa kutumia nilicho nacho, na hata kujitolea mimi mwenyewe kabisa, kwa faida ya roho zenu. Je, mtanipenda kidogo ati kwa kuwa mimi nawapenda ninyi mno?
une nili nu lukeelo kuhumia ifiiu fyango na kukuhumia juune kukuvatanga umue. nave nikuvaghana fiijo, ninoghiile kughanua padebe?
16 Basi, mtakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu. Lakini labda mtu mwingine atasema: “Kwa vile Paulo ni mwerevu, amewafanyieni ulaghai.”
neke ndavule lulivuo, une nanikaale n'sigho kulyumue. looli ulwakuva une nili n'sufu fiijo, nihwene juno avakoovile nu vusyangi.
17 Je, mimi niliwanyonyeni kwa njia ya mjumbe yeyote niliyemtuma kwenu?
asi! nikatoliile kimonga kulyumue mulwa kukava uluvumbulilo kukilila avaanhu vano nikavasung'hile?
18 Mimi nilimwita Tito, nikamtuma kwenu na ndugu yetu mwingine. Je, Tito aliwanyonyeni? Je, hamjui kwamba sisi tumekuwa tukiongozwa na roho yuleyule, na mwenendo wetu ni mmoja?
nikan'sumile uTiito palikimo nu nyalukolo ghwitu ujunge kuuti iise kulyumue. asi! uTiito akatoolile kimoga kulyumue? asi! natukagwile musila jila jila? vule, natukaghendile mu sajo sila sila?
19 Labda mnafikiri kwamba mpaka sasa tumekuwa tukijitetea wenyewe mbele yenu! Lakini, tunasema mambo haya mbele ya Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo. Mambo hayo, yote, wapenzi wangu, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
musagha kuuti un'siki ghwoni ughu, tukujooleka kulyumue kuuti muleke pikutuvona kuuti tulivavivi pa maaso ghiinu? tujova isi ulwakuva tuli vavombi va Kilisite, na ju Nguluve akagwile, isi sooni tuvomba kukuvatanga mukangale mu lwitiko.
20 Naogopa, huenda nitakapokuja kwenu nitawakuta katika hali nisiyopenda, nami itanilazimu kuwa katika hali msiyoipenda. Naogopa huenda kukawa na ugomvi, wivu, uhasama, ubishi, masengenyano, kunong'ona, majivuno na fujo kati yenu.
lino nikwoghopa kuuti, niliiva nikwisa kulyumue nili kuvagha muli nu luveelo luno nanikeela une. nikwoghopa kuuti ndepoonu nilikuvaagha muli na mabaatu, ni giila, ni ng'halaasi, nu vusulani, kudeselanila kukughinia kuuva na matiling'hano.
21 Naogopa huenda hapo nitakapokuja safari ijayo Mungu wangu atanifanya niaibike mbele yenu, nami nitaomboleza kwa ajili ya wengi wa wale waliotenda dhambi lakini hawakujutia huo uchafu, tamaa zao mbaya na uzinzi waliokuwa wamefanya.
kange nikwoghopa kuuti niliiva nikwiisa kulyumue, uNguluve ghwango ilikumbiika nivone soni pa maaso ghiin. nilisukunala kuvona avaanhu vinga mulyumue vano vakavombile inyivi ulutasi, navalatile. vajighe na maghendele agha vuvwafu, uvughendamwalu nu vunoghelua uvunge vuno vakaale navwo.

< 2 Wakorintho 12 >