< Matendo 9 >

1 Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
But Saul, still breathing threat and slaughter against the disciples of the Lord, after going to the high priest,
2 akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
he requested letters from him for Damascus, to the synagogues, so that if he found any who were of the Way, both men and women, he might bring them bound to Jerusalem.
3 Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
And on going, it came to pass for him to approach Damascus. And suddenly there shone around him a light out of heaven.
4 Akaanguka chini na kusikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?”
And after falling to the ground, he heard a voice saying to him, Saul, Saul, why do thou persecute me?
5 Naye Saulo akauliza, “Ni nani wewe Bwana?” Na ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
And he said, Who are thou, Lord? And the Lord said, I am Jesus whom thou persecute.
6 Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”
But arise, and enter into the city, and it will be told thee what thou must do.
7 Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
And the men who traveled with him had stopped, speechless, indeed hearing the voice, but seeing no man.
8 Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
And Saul arose from the ground. And when his eyes were opened, he saw no man. But they brought him into Damascus, leading him by the hand.
9 Saulo alikaa siku tatu bila kuona, na wakati huo hakula au kunywa chochote.
And he was three days not seeing, and did not eat or drink.
10 Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, “Anania!” Anania akaitika, “Niko hapa, Bwana.”
Now there was a certain disciple in Damascus, named Ananias, and the Lord said to him in a vision, Ananias. And he said, Behold me, Lord.
11 Naye Bwana akamwambia, “Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
And the Lord said to him, After rising, go into the street called Straight, and seek in the house of Judas, a man named Saul of Tarsus, for behold, he is praying.
12 na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena.”
And he saw in a vision a man named Ananias who came in and laid a hand on him, so that he might receive sight.
13 Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
But Ananias answered, Lord, I have heard from many about this man, how many evil things he did to thy sanctified at Jerusalem.
14 Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako.”
And here he has authority from the chief priests to bind all who call upon thy name.
15 Lakini Bwana akamwambia, “Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
But the Lord said to him, Go, because this man is a chosen vessel to me, to bear my name before Gentiles and kings, and sons of Israel.
16 Mimi mwenyewe nitamwonyesha mengi yatakayomlazimu kuteswa kwa ajili ya jina langu.”
For I will give him a glimpse of how many things it is necessary for him to suffer for my name.
17 Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, “Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu.”
And Ananias departed and entered into the house. And having laid hands on him he said, Brother Saul, the Lord, he who appeared to thee on the road on which thou came, has sent me so that thou may receive sight, and be filled of the Holy Spirit.
18 Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
And straightaway there fell from his eyes, like scales, and he looked up. And immediately after rising up, he was immersed.
19 Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
And having received nourishment, he was strengthened. And Saul became with the disciples in Damascus some days.
20 Mara alianza kuhubiri katika masunagogi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
And straightaway he proclaimed the Christ in the synagogues, that this man is the Son of God.
21 Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, “Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!”
And all those who heard were amazed, and said, Is this not the man who destroyed those in Jerusalem who call on this name? And he has come here for this, so that he might bring them bound to the chief priests.
22 Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
But Saul was strengthened more, and was confounding the Jews who dwell at Damascus, proving that this is the Christ.
23 Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi walikusanyika na kufanya mpango wa kumwua Saulo.
And after considerable days were fulfilled, the Jews plotted to destroy him,
24 Lakini Saulo alipata habari ya mpango huo. Usiku na mchana walilinda milango ya kuingia mjini ili wapate kumwua.
but their plot was known to Saul. And they watched the gates both day and night so that they might destroy him.
25 Lakini wakati wa usiku wanafunzi wake walimchukua, wakamteremsha chini ndani ya kapu kubwa kwa kupitia nafasi iliyokuwako ukutani.
But the disciples, after taking him by night, let him down through the wall, having lowered him in a hamper.
26 Saulo alipofika Yerusalemu alijaribu kujiunga na wale wanafunzi. Lakini wote walimwogopa, na hawakuweza kuamini kwamba yeye amekuwa mfuasi.
And when Saul arrived in Jerusalem, he attempted to join with the disciples, and they all feared him, not believing that he is a disciple.
27 Hapo, Barnaba alikuja akamchukua Saulo, akampeleka kwa mitume na kuwaeleza jinsi Saulo alivyomwona Bwana njiani na jinsi Bwana alivyoongea naye. Aliwaambia pia jinsi Saulo alivyokuwa amehubiri bila uoga kule Damasko.
But Barnabas having taken him, he brought him to the apostles. And he related to them how he saw the Lord on the road, and that he spoke to him, and how he spoke boldly at Damascus in the name of Jesus.
28 Basi, Saulo alikaa pamoja nao, akatembelea Yerusalemu yote akihubiri neno la Bwana bila hofu.
And he was with them coming in and going out at Jerusalem, and speaking boldly in the name of the Lord Jesus.
29 Pia aliongea na kubishana na Wayahudi wasemao Kigiriki, lakini wao walijaribu kumwua.
And he spoke and disputed against the Hellenists, but they attempted to destroy him.
30 Wale ndugu walipogundua jambo hilo walimchukua Saulo, wakampeleka Kaisarea, wakamwacha aende zake Tarso.
But when the brothers knew it, they brought him down to Caesarea, and sent him away to Tarsus.
31 Wakati huo kanisa likawa na amani popote katika Yudea, Galilaya, na Samaria. Lilijengwa na kukua katika kumcha Bwana, na kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
Indeed therefore the congregations throughout the whole of Judea and Galilee and Samaria had peace, being edified. And, going in the fear of the Lord and in the encouragement of the Holy Spirit, they were multiplied.
32 Petro alipokuwa anasafirisafiri kila mahali alifika pia kwa watu wa Mungu waliokuwa wanaishi Luda.
And it came to pass, Peter, passing through all parts, to also come down to the sanctified who dwell at Lydda.
33 Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Enea ambaye kwa muda wa miaka minane alikuwa amelala kitandani kwa sababu alikuwa amepooza.
And he found there a certain man named Aeneas, who was paralyzed, laying on a bed for eight years.
34 Basi, Petro akamwambia, “Enea, Yesu Kristo anakuponya. Amka utandike kitanda chako.” Enea akaamka mara.
And Peter said to him, Aeneas, Jesus the Christ heals thee. Arise and make thy bed. And straightaway he arose.
35 Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Enea, na wote wakamgeukia Bwana.
And all those dwelling at Lydda and Sharon who saw him, turned to the Lord.
36 Kulikuwa na mfuasi mmoja mwanamke mjini Yopa aitwaye Tabitha (kwa Kigiriki ni Dorka, maana yake, Paa). Huyo mwanamke alikuwa akitenda mema na kuwasaidia maskini daima.
Now at Joppa there was a certain disciple named Tabitha, which, being translated, is called Dorcas. This woman was full of good works and charities that she did.
37 Wakati huo ikawa kwamba aliugua, akafa. Watu wakauosha mwili wake, wakauzika katika chumba ghorofani.
And in those days, having been ill, she happened to die. And after washing her, they laid her in an upper chamber.
38 Yopa si mbali sana na Luda; kwa hiyo wafuasi waliposikia kwamba Petro alikuwa Luda, wakawatuma watu wawili kwake na ujumbe: “Njoo kwetu haraka iwezekanavyo.”
And since Lydda is near Joppa, the disciples, having heard that Peter is in it, they sent two men to him, exhorting him not to delay to go through to them.
39 Basi, Petro akaenda pamoja nao. Alipofika alipelekwa ghorofani katika kile chumba. Huko wajane wengi walimzunguka Petro wakilia na kumwonyesha makoti na nguo ambazo Dorka alikuwa akitengeneza wakati alipokuwa hai.
And after rising, Peter went with them, whom, after coming, they brought into the upper chamber. And all the widows stood by him weeping, and exhibiting the coats and garments, as many things as Dorcas made being with them.
40 Petro aliwatoa nje wote, akapiga magoti, akasali. Kisha akamgeukia yule maiti, akasema, “Tabitha, amka” Naye akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
But Peter, having sent them all out, having knelt down, he prayed. And having turned to the body, he said, Tabitha, arise. And the woman opened her eyes. And when she saw Peter, she sat up.
41 Petro akamsaidia kusimama, halafu akawaita wale watu wa Mungu na wale wajane, akamkabidhi kwao akiwa mzima.
And having given her a hand, he raised her up. And after calling the sanctified and the widows, he presented her alive.
42 Habari ya tukio hili ilienea kila mahali huko Yopa, na watu wengi wakamwamini Bwana.
And it became known throughout the whole of Joppa, and many believed in the Lord.
43 Petro alikaa siku kadhaa huko Yopa, akiishi kwa mtu mmoja mtengenezaji wa ngozi aitwaye Simoni.
And it came to pass for him to remain considerable days at Joppa with a certain Simon, a tanner.

< Matendo 9 >