< Waefeso 6 +

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
Children, do what your parents tell you, for this is the right thing to do.
2 “Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
“Honor your father and mother.” This is the first commandment that has a promise attached:
3 “Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
“that things may go well for you and you may live a long life on the earth.”
4 Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
Fathers, don't make your children mad, but look after them by disciplining them and instructing them about God.
5 Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
Servants, obey those who are your human masters, with proper respect and awe, doing things from sincere motives as if you were serving Christ.
6 Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
Don't just work well when you're being watched to gain approval, but work like servants of Christ, honestly doing God's will,
7 Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
happily serving as if you were doing it for the Lord, and not for people.
8 Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
You know that whoever does what's good will be rewarded by the Lord, whether that person is a servant or someone who is free.
9 Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
Masters, you should treat your servants the same way. Don't threaten them, remember that the Lord in heaven is both their master and yours, and he treats people the same, without favoritism.
10 Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
Lastly, stay strong in the Lord, and in his mighty power.
11 Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
Put on all the armor of God so you can withstand all the devil's attacks!
12 Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn g165)
We're not fighting against human forces, but against supernatural rulers and powers, the dark lords of this world, against the spiritual forces of evil in the heavens. (aiōn g165)
13 Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
Take all the weapons God provides so that you may be able to stand your ground in the day of evil and after doing all you can, to find yourself still standing!
14 Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
So stand up, wrap the belt of truth around your waist, tie on the breastplate of justice and the right,
15 na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
and put on the shoes of readiness to share the good news of peace.
16 Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
Above all, take up the shield of trusting God, by which you'll be able to put out all the devil's flaming arrows.
17 Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
Wear the helmet of salvation, and carry the sword of the Spirit—the Spirit that's the word of God.
18 Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
Always pray in the Spirit as you do all this. Stay awake and keep on praying for all God's people.
19 Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
Pray for me too so that I'll be given the right words to say, and that I'll be able to explain confidently the hidden truths of the good news.
20 Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
I'm an imprisoned ambassador for the sake of the good news, so please pray that I will speak fearlessly, as I should.
21 Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
Tychicus, our good friend and faithful minister, will give you all my news and explain everything so you'll know how I'm doing.
22 Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
That's why I'm sending him to you—to tell you what's happened to us and to encourage you.
23 Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
Peace to all the Christians there, from God the Father and the Lord Jesus Christ, with love and trust in him.
24 Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
Grace to all those who eternally love our Lord Jesus.

< Waefeso 6 +