< Yohana 13 >

1 Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
Now before the feast of the Passover, Jesus knew that his hour had come to depart from this world and go to the Father. Having loved his own who were in the world, he loved them to the end.
2 Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
By the time supper ended, the devil had put it into the heart of Judas Iscariot, the son of Simon, to betray Jesus.
3 Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
Jesus knew that the Father had put all things into his hands, and that he had come from God and was going back to God,
4 Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
so he rose from supper, laid aside his outer garments, took a towel, and wrapped it around his waist.
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
After that, he put water into the washbasin and began to wash his disciples' feet and to wipe them with the towel that was wrapped around his waist.
6 Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
When he came to Simon Peter, Peter said to him, “Lord, are yoʋ going to wash my feet?”
7 Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
Jesus answered him, “What I am doing yoʋ do not now understand, but afterward yoʋ will understand.”
8 Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn g165)
Peter said to him, “Yoʋ shall never wash my feet.” Jesus answered him, “If I do not wash yoʋ, yoʋ have no part with me.” (aiōn g165)
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
Simon Peter said to him, “Lord, then wash not only my feet, but also my hands and my head.”
10 Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
Jesus said to him, “He who has bathed has no need to wash, except for his feet, but is completely clean. And you are clean, but not all of you.”
11 (Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
(For he knew who would betray him; that is why he said, “You are not all clean.”)
12 Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
When Jesus had washed their feet and collected his garments, he reclined again at the table and said to them, “Do you know what I have done for you?
13 Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
You call me Teacher and Lord, and rightly so, for that is what I am.
14 Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
So if I, your Lord and Teacher, have washed your feet, you also ought to wash one another's feet.
15 Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
For I have given you an example so that you should do as I have done for you.
16 Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
Truly, truly, I say to you, a servant is not greater than his master, nor is a messenger greater than the one who sent him.
17 Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
If you know these things, you are blessed if you do them.
18 “Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
I am not speaking about all of you; I know those whom I have chosen for myself. But the Scripture must be fulfilled: ‘He who eats bread with me has lifted up his heel against me.’
19 Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
I am telling you now before it happens, so that when it does happen, you will believe that I am he.
20 Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
Truly, truly, I say to you, whoever receives the one I send receives me, and whoever receives me receives him who sent me.”
21 Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
After saying these things, Jesus was troubled in his spirit and declared, “Truly, truly, I say to you, one of you will betray me.”
22 Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
So the disciples began looking at one another, perplexed as to whom he was speaking about.
23 Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
One of his disciples, the one whom Jesus loved, was reclining on Jesus' chest.
24 Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
So Simon Peter motioned to him to ask Jesus whom he was talking about.
25 Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
Leaning back on Jesus' chest, he said to him, “Lord, who is it?”
26 Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
Jesus answered, “It is the one to whom I give this morsel after I have dipped it.” Then he dipped the morsel and gave it to Judas Iscariot, the son of Simon.
27 Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
After Judas took the morsel, Satan entered into him. Then Jesus said to him, “What yoʋ are about to do, do quickly.”
28 Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
(Now none of those reclining at the table knew why he said this to him.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
Some were thinking, since Judas had the moneybag, that Jesus was saying to him, “Buy what we need for the feast,” or that he should give something to the poor.)
30 Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
As soon as Judas took the morsel, he went out. And it was night.
31 Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
When Judas had gone out, Jesus said, “Now the Son of Man is glorified, and God is glorified in him.
32 Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
If God is glorified in him, God will also glorify the Son in himself, and will glorify him immediately.
33 “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
Little children, I am with you for a little while longer. You will seek me, and just as I said to the Jews, now I say to you also, ‘Where I am going, you cannot come.’
34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
I give you a new commandment, that you love one another. Just as I have loved you, so you must love one another.
35 Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
By this everyone will know that you are my disciples, if you have love for one another.”
36 Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter said to him, “Lord, where are yoʋ going?” Jesus answered him, “Yoʋ cannot follow me now to the place where I am going, but afterward yoʋ will follow me.”
37 Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
Peter said to him, “Lord, why can I not follow yoʋ now? I will lay down my life for yoʋ.”
38 Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”
Jesus answered him, “Yoʋ will lay down yoʋr life for me? Truly, truly, I say to yoʋ, a rooster will certainly not crow until yoʋ have denied me three times.”

< Yohana 13 >