< Ufunuo 18 >

1 Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
Après cela, je vis descendre du ciel un autre ange qui avait une grande puissance, et la terre était illuminée de sa gloire,
2 Basi, akapaaza sauti kwa nguvu akisema, “Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
et il cria d'une voix formidable: «Elle est tombée, elle est tombée, la grande Babylone, elle est devenue une demeure de démons, un refuge d'Esprits impurs, un refuge d'oiseaux immondes et détestés,
3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”
parce que toutes les nations ont bu du vin de feu de sa fornication, et que les rois de la terre ont forniqué avec elle, et que les marchands de la terre se sont enrichis de son opulence.»
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema, “Watu wangu, ondokeni kwake, ili msishirikiane naye katika dhambi zake, msije mkaipata adhabu yake.
Et j'entendis une autre voix qui venait du ciel et disait: «Sortez d'elle, ô mon peuple, pour ne pas vous rendre complices de ses péchés et pour n'être pas atteints par les plaies qui vont la frapper.
5 Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
Ses péchés se sont accumulés jusqu'au ciel, et Dieu s'est souvenu de ses iniquités.
6 Mtendeeni kama alivyowatendea ninyi; mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda. Jazeni kikombe chake kwa kinywaji kikali mara mbili zaidi ya kile alichowapeni.
Faites-lui ce qu'elle a fait aux autres; payez-la au double de ses oeuvres, versez-lui à boire le double de la coupe qu'elle a versée aux autres.
7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!
Autant elle a eu de gloire et d'opulence, autant donnez-lui de tourment et d'affliction. «Je suis assise en reine, dit-elle en son coeur, je ne suis pas' veuve, et je ne connaîtrai jamais le deuil.»
8 Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja: ugonjwa, huzuni na njaa. Atachomwa moto, maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ni Mwenye Uwezo.”
Voilà pourquoi toutes ses plaies viendront en un même jour, mort, et désolation, et famine, et destruction par le feu, car puissant est le Seigneur Dieu qui l'a jugée.»
9 Wafalme wa Dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
Et l'on verra pleurer et se lamenter sur elle les rois de la terre qui ont forniqué avec elle et ont eu leur part de son opulence. A la vue de la fumée de son embrasement
10 Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake, na kusema, “Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata.”
et se tenant à distance par crainte de ses tourments: «Malheur! malheur! diront-ils, Quoi! la grande ville! Babylone! la puissante ville! en une heure est venu ton jugement!»
11 Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;
Et les marchands de la terre pleureront et se désoleront sur elle, car personne n'achète plus leurs marchandises:
12 hakuna tena wa kununua dhahabu yao, fedha, mawe ya thamani na lulu, kitani na nguo za rangi ya zambarau, hariri na nguo nyekundu; vyombo vya kila aina ya miti ya pekee, vyombo vya pembe za ndovu, vya miti ya thamani kubwa, vya shaba, chuma na marmari;
marchandises d'or et d'argent, et pierres précieuses, et perles, et fin lin, et pourpre, et soie, et écarlate, et bois de thuia, et objets en ivoire, et objets en bois précieux, et en bronze, et en fer, et en marbre;
13 mdalasini, viungo, ubani, manemane, udi, divai, mafuta, unga na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari ya kukokotwa, watumwa wao na hata maisha ya watu.
et cinname, et amome, et parfums, et huiles aromatiques, et encens, et vin, et huile, et fleur de farine, et froment, et boeufs, et brebis, et chevaux, et chars, et corps et âmes d'hommes.
14 Wafanyabiashara wanamwambia: “Faida yote uliyotazamia imetoweka, na utajiri na fahari vimekuponyoka; hutaweza kuvipata tena!”
Et toute cette moisson de choses que convoitait ton âme s'en est allée loin de toi, et toutes ces choses brillantes et magnifiques sont perdues pour toi, et tu ne le trouveras plus jamais.
15 Wafanya biashara waliotajirika kutokana na mji huo, watasimama mbali kwa sababu ya hofu ya mateso yake, watalalamika na kuomboleza,
Les marchands de toutes ces choses qui se sont enrichis par elles, se tenant à distance par crainte de ses tourments, pleurant
16 wakisema, “Ole! Ole kwa mji huu mkuu. Ulizoea kuvalia nguo za kitani, za rangi ya zambarau na nyekundu, na kujipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu!
et se désolant: «Malheur! malheur! diront-ils, Quoi! la grande ville vêtue d'écarlate, et de pourpre, et de fin lin, parée d'or et de pierres précieuses et de perles!
17 Kwa saa moja tu utajiri wako umetoweka!” Halafu manahodha wote na wasafiri wao, wanamaji na wote wanaofanya kazi baharini, walisimama kwa mbali,
En une heure ont péri tant de richesses!» Et les pilotes et les marins qui venaient vers elle, et les matelots, et tous ceux qui trafiquent de la mer, s'arrêtant à distance,
18 na walipouona moshi wa moto ule uliouteketeza, wakalia kwa sauti: “Hakujapata kuwako mji kama mji huu mkuu!”
se répandent en cris à la vue de la fumée de son incendie: «Quelle ville, disent-ils, égalait la grande ville?»
19 Wakajimwagia vumbi juu ya vichwa vyao wakilia kwa sauti na kuomboleza: “Ole! Ole kwako mji mkuu! Ni mji ambamo wote wenye meli zisafirizo baharini walitajirika kutokana na utajiri wake. Kwa muda wa saa moja tu umepoteza kila kitu!”
et ils jettent de la poussière sur leur tête et se répandent en cris, en pleurs, et en lamentations. «Malheur! malheur! disent-ils, grande ville qui enrichissait de ses trésors tous ceux qui avaient des vaisseaux sur la mer; en une seule heure elle a été changée en désert!»
20 Furahi ee mbingu, kwa sababu ya uharibifu wake. Furahini watu wa Mungu, mitume na manabii! Kwa maana Mungu ameuhukumu kwa sababu ya mambo uliyowatenda ninyi!
Réjouis-toi de sa ruine, ô ciel; et vous, les saints, et les apôtres, et les prophètes, réjouissez-vous, car Dieu a vengé votre cause sur elle.»
21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu sana akainua jiwe mfano wa jiwe kubwa la kusagia, akalitupa baharini akisema, “Ndivyo, Babuloni atakavyotupwa na kupotea kabisa.
Et un ange d'une force extraordinaire prit une pierre grosse comme une meule et la lança dans la mer en disant: «C'est avec cette violence que sera précipitée Babylone, la grande ville, et on ne la retrouvera plus jamais.
22 Sauti za vinubi za muziki, sauti za wapiga filimbi na tarumbeta hazitasikika tena ndani yako. Hakuna fundi wa namna yoyote ile atakayepatikana tena ndani yako; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikika tena ndani yako.
Et la voix des joueurs de harpe, et des musiciens, et des joueurs de flûte et de trompette ne résonnera plus dans tes murs; ni artisan, ni métier ne se trouvera désormais chez toi;
23 Mwanga wa taa hautaonekana tena ndani yako; sauti za bwana arusi na bibi arusi hazitasikika tena ndani yako. Wafanyabiashara wako walikuwa wakuu duniani, na kwa uchawi wako mataifa yote yalipotoshwa!”
le bruit de la meule ne s'y fera point entendre; la lumière de la lampe n'y brillera plus jamais; et la voix du fiancé et celle de la fiancée ne s'y feront plus entendre; car tes marchands étaient les grands de la terre, et ce sont tes enchantements qui ont égaré toutes les nations,
24 Mji huo uliadhibiwa kwani humo mlipatikana damu ya manabii, damu ya watu wa Mungu na damu ya watu wote waliouawa duniani.
et c'est là qu'on a trouvé le sang des prophètes, et des saints, et de tous ceux qui ont été égorgés sur la terre.

< Ufunuo 18 >