< Tito 1 >

1 Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
Paul, serviteur de Dieu, apôtre de Jésus-Christ, pour annoncer la foi des élus de Dieu, pour faire connaître la vérité conforme a la piété
2 ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios g166)
et donner l'espérance de la vie éternelle, promise depuis un temps immémorial par le Dieu véridique, (aiōnios g166)
3 na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
révélée au temps marqué par sa parole dont il a donné l'ordre de me confier la prédication, lui, notre Dieu sauveur,
4 Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
à Tite, mon véritable enfant dans la foi qui nous est commune. Grâce et paix te soient données par Dieu notre Père et par Jésus-Christ notre Seigneur.
5 Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
Voici pourquoi je t'ai laissé en Crète: pour que tu règles ce qui reste à régler et que, dans chaque ville, tu installes des Anciens aux conditions que je t'ai indiquées:
6 mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
être sans reproche, mari d'une seule femme, avoir des enfants croyants, qui ne soient ni indisciplinés, ni accusés de vivre dans le désordre.
7 Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
Oui, le conducteur d'une Église doit être sans reproche, étant l'intendant de Dieu; il ne doit être ni insolent, ni colère; n'aimer ni le vin ni les querelles; ne pas être bassement intéressé;
8 Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
mais être hospitalier, aimer à faire le bien; être modéré, juste, pieux, sobre,
9 Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
attaché à la parole authentique, conformément à la doctrine reçue, pour être capable, lui aussi, d'exhorter par un sain enseignement et de réfuter les contradicteurs.
10 Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
Car ils sont nombreux, surtout parmi les circoncis, les indisciplinés, les bavards, les trompeurs
11 Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
auxquels il faut fermer la bouche. Ces gens-là mettent le désordre dans des familles entières, enseignant ce qu'il ne faut pas enseigner et cela par honteux intérêt.
12 Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: “Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!”
Un des leurs a été leur propre prophète quand il a dit: «...Crétois, toujours menteurs, vilaines bêtes, ventres paresseux...»
13 Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
Voilà un jugement mérité; voilà le motif de les reprendre sévèrement, pour qu'ils aient une foi saine,
14 Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
qu'ils ne s'occupent pas de contes judaïques et de commandements d'hommes abandonnant la vérité.
15 Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
Tout est pur pour ceux qui sont purs; quant aux corrompus et aux incrédules, rien ne leur est pur; leurs pensées et leurs consciences sont corrompues.
16 Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.
Ils prétendent connaître Dieu, et leurs oeuvres le renient; ils sont abominables, rebelles, incapables de rien faire de bien.

< Tito 1 >