< Малахії 1 >

1 Пророцтво Господнього слова до Ізраїля через Малахі́ю.
Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.
2 „Я вас полюбив, — говорить Госпо́дь, — а ви кажете: „Як Ти нас полюбив?“Чи ж не брат Іса́в Якову? каже Госпо́дь, а Я Якова був полюбив,
Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.” “Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’” Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo,
3 а Іса́ва знена́видів, і зробив його гори спусто́шенням, а спа́док його — для шака́лів пустині.
lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
4 Коли скаже Едо́м: „Ми зруйно́вані, та зно́ву збуду́ємо руїни“, то так промовляє Госпо́дь Савао́т: Вони побуду́ють, а Я розвалю́! І звати їх будуть: Країна безбо́жности, і наро́д, на якого навіки розгні́вавсь Господь!
Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.” Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana.
5 І ваші очі побачать оце, і ви скажете: Стане великий Госпо́дь понад границю Ізраїлеву!
Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’
6 Шанує син ба́тька, а раб — свого пана; та якщо Я вам ба́тько, де пошана Моя? А якщо Я вам пан, де страх передо Мною? говорить Господь Савао́т вам, священики, що пого́рджуєте Моїм Іме́нням та й кажете: „Чим ми погорди́ли Йме́нням Твоїм?“
“Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu. “Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’
7 На же́ртівник Мій ви прино́сите хліб занечи́щений і кажете: „Чим Тебе ми знева́жили?“Тим, що кажете ви: „Трапе́за Господня — вона пого́рджена!“
“Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu. “Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’ “Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa.
8 І коли ви прино́сите в жертву сліпе́, це не зле? І як кульга́ве та хворе прино́сите, чи ж це не зле? Принеси но поді́бне своє́му намі́сникові, чи тебе він вподо́бає, чи піді́йме обличчя твоє? промовляє Госпо́дь Савао́т.
Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 А тепер ублага́йте ви Боже лице, і хай стане для нас милости́вим, з ваших рук це було́, то хіба кому з вас Він обличчя піді́йме? говорить Господь Саваот.
“Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
10 Нехай хто серед вас замкне двері святині, і не бу́де нада́рмо освічувати Мого же́ртівника! Я не маю вподо́би до вас, говорить Господь Савао́т, і з ваших рук не вподо́баю да́ру!
“Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu.
11 Бо від сходу сонця й аж по за́хід його́ звеличи́ться Йме́ння Моє між наро́дами, і ка́диться в кожному місці для Ймення Мого дар чистий, бо звели́читься Ймення Моє між наро́дами, каже Госпо́дь Савао́т.
Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
12 Ви ж Його зневажа́єте, ка́жучи: „Трапе́за Господня — вона занечи́щена, й дохід її, обри́джена страва її“.
“Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’
13 І до того говорите: „Ось стільки пра́ці!“і ним нехтуєте, — говорить Госпо́дь Савао́т, — і прино́сите кра́дене, і кульга́ве та хворе, і таку жертву хлібну прино́сите. Чи буде воно Мені миле з рук ваших? говорить Госпо́дь.
Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana.
14 І прокля́тий обма́нець, що в ста́ді його є саме́ць, а він обіцяє та в жертву дає Господе́ві зіпсуте, А Я Цар великий, — говорить Госпо́дь, — і серед наро́дів грізне́ Моє Ймення!
“Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

< Малахії 1 >